WILSON KOLINA ELISHA

WILSON KOLINA ELISHA

BLOG HII NI MUHIMU KWA JAMII KUTOKANA NA KUJIKITA KATIKA KUANDIKA HABARI TOFAUTI ZA UHAKIKA NA ZILIZOFANYIWA UCHAMBUZI WA KINA...........

Thursday, October 3, 2013

GERFA YAPATA UDHAMINI: ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 16 KUTUMIKA LIGI YA MKOA GEITA

MKATABA SOKA GEITA
Na Wilson Elisha
Geita
03/10/2013

Chama cha soka Mkoa wa Geita GERFA kimetiliana saini mkataba wa kudhamini ligi ya mkoa huo hatua ya Nane bora  baina ya Taasisi ya Mtalitinya Foundation  kwa kipindi cha misimu miwili kuanzia mwaka 2013/2014 hadi 1015 wenye thamani ya zaidi ya shilingi Milioni 16.

Mkataba huo utajikita katika kuvumbua, kukuza na kuendeleza  vipaji vya vijana katika michezo sanjari na masuala ya Maendeleo, uchumi  Afya na Ukimwi.

Hafla fupi ya kutiliana saini mkataba  wa udhamini wa ligi ya Mkoa wa Geita ambayo imehudhuriwa na wadau mbalimbalu kutoka mkoani humo imefanyika katika Ukumbi wa Nkola ulioko Mjini Geita.

Mgeni rasmi katika hafla hiyo Kamanda wa Polisi mkoa wa Geita  Leonard Paulo amesema udhamini huo umetolewa na mdau mwelevu ambaye anathamini na kutambua umuhimu wa maendeleo hivyo ni vema wadau wengine wakaunga mkono jitihada hizo ili kuweza kupata manufaa zaidi na kufikia malengo ya kundeleza michezo.


Kwa upande wake mdhamini  mkuu wa ligi hiyo ya Mkoa wa Geita kupitia Taasisi yake ya Mtalitinya Foundation , Jacob Mtalitinya amewatahadharisha viongozi wa vyama
vya michezo kuachana na tabia ya kujikita katika migogoro na kuleta ugomvi badala ya kujikita katika mipango ya kuwaletea maendeleo wanamichezo.

Mwenyekiti wa chama cha soka Mkoa wa  Geita GERFA, Salum Kulunge amesema anaamini kuwa kusainiwa kwa makataba huo ni historia katika mkoa  huo ikiwa ni mwaka mmoja tangu waingie madarakani mOktoba mwaka jana 2012.

Amebainisha kuwa mkataba huo ni mkubwa sana hivyo chama chake kinampongeza mdhamini mkuu wa ligi ya Mkoa wa Geita na kuwaomba wadau wauunge mkono na si kuubeza kwani zipo ligi nyingi katika mikoa ya Tanzania Bara na Zanzibar hawajapata wadhaminnji wa ligi zao.

Mratibu wa Taasisi ya Vijana na maendeleo ya Mtalitinya Foundation  ambayo imedhamini ligi hiyo David Azaria amesema kuwa washindi watazawadiwa zawadi mbalimbali ikiwemo kombe na fedha taslimu  Az
VOX:2
1.Salum Kulunge – M/Kiti GEDFA
2.David Azaria – Mratibu wa Mtalitinya Foundation
Mkataba huo utazihusisha jumla ya timu Nane ambazo zitatinga katika hatua ya robo fainali kwa kipindi cha misimu miwili  huku bingwa akizawadiwa kombe na kitita cha shilingi Milioni moja, mshindi wa pili shilingi Laki tano na mshindi wa tatu shilingi laki mbili na nusu.
Mwisho

SIGN OFF

No comments:

Post a Comment