WILSON KOLINA ELISHA

WILSON KOLINA ELISHA

BLOG HII NI MUHIMU KWA JAMII KUTOKANA NA KUJIKITA KATIKA KUANDIKA HABARI TOFAUTI ZA UHAKIKA NA ZILIZOFANYIWA UCHAMBUZI WA KINA...........

Tuesday, January 13, 2015

MPANGO WA TASAF 3 WA KUSAIDIA KAYA MASKINI WAZINDULIWA WILAYANI NYANG'HWALE MKOANI GEITA


Suala la kubaini kaya maskini nchini linalotokana na mpango wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF awamu ya tatu linapaswa kufanyika kwa umakini ili kuondoa migogoro na utata unaoweza kujitokeza katika jamii.

Hii itasaidia walengwa waliokusudiwa kunufaika kutokana na ukweli kwamba zipo kaya nyingi nchini ambazo ni maskini lakini zinazotarajiwa kunufaika na mpango huo ni zaidi ya kaya miloni moja.


Mkuu wa wilaya ya Nyang'hwale Mkoani Geita Ibrahim Marwa akisisitiza jambo kwa wajumbe wakati wa kikao elekezi cha kubaini kaya maskini.
Tatu Mwaruka Afisa wa kuboresha Maisha ya Jamii  TASAF  Makao makuu akielezea wajumbe wa wilaya ya Nyang'hwale Mkoani  Geita  namna walivyojipanga katika awamu hii.


Mhandisi Barnabas Jachi Kamu meneja wa miradi ya Kutoa ajira  makao makuu TASAF  ambaye  pia ni mtaalam wa mazingira


Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Nyang'hwale Fortunata Malya akisimama kuelezea furaha yake kupokea mpango huu wa TASAF 3 wa kunusuru kaya maskini katika wilaya hiyo.






 Baadhi ya wajumbe wa kikao elekezi cha Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF 3 cha namna ya  kubaini kaya maskini katika wilaya ya Nyang'hwale Mkoani Geita wakimsikiliza Mkuu wa wilaya hiyo Ibrahim Marwa hayupo pichani wakati akifungua kikao hicho


Mkuu wa wilaya ya Nyang’hwale Mkoani Geita Ibrahim Marwa ametoa kauli hiyo wakati wa uzinduzi wa mpango wa TASAF awamu ya tatu wilayani huo.



Amesema ana amini kuwa viongozi ambao wamepewa jukumu la kusimamia  katika kubaini kaya maskini watazingatia taratibu , kanuni na vigezo ambavyo vimewekwa ili walengwa wanufaike.





Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi mkuu wa TASAF  Taifa  Kaimu meneja miradi ya kutoa ajira ambaye pia ni mtaalam wa mazingira kutoka makao makuu ya TAFAS  mhandisi Barnabas Jachi anaelezea yaMNA YA  kubaini kaya maskini ili ziweze kunufaika na mpango huo.



     
Mratibu wa TASAF wilaya ya Nang’hwale Nashon Magumba na baadhi ya wajumbe  ambao wameshiriki katika uzinduzi huo ambao umeambatana na mafunzo ya namna ya kuzitambua kaya maskini wanaelezea jinsi ambavyo wameupokea mpango huo.

Mpango wa TASAF awamu ya tatu katika wilaya ya Nyang’hwale Mkoani Geita  utavinufaisha vijiji 40 kati ya 62 ,   kaya zaidi 2, 500 katika awamu hii.

Mwisho

No comments:

Post a Comment