WILSON KOLINA ELISHA

WILSON KOLINA ELISHA

BLOG HII NI MUHIMU KWA JAMII KUTOKANA NA KUJIKITA KATIKA KUANDIKA HABARI TOFAUTI ZA UHAKIKA NA ZILIZOFANYIWA UCHAMBUZI WA KINA...........

Tuesday, January 13, 2015

MARA QUEENS WAMALIZA KAMBI, KUKIPUTA LEO NA MWANZA QUEENS MKOANI MARA



Kufuatia kipigo cha mabao sita kwa moja kutoka kwa timu ya soka ya Mwanza Queen katika masshindano ya kombe la Taifa kwa wanawake timu ya soka ya wanawake ya Mkoa wa Mara imeweka kambi kwa ajili ya kulipiza kisasa katika mchezo wa marudiano.

Timu hiyo ya wanawake ya Mkoa wa Mara imeweka kambi jijini Mwanza ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya kulipa kisasi ili iweze kusonga mbele katika mashindano hayo.
 Ni  wachezaji wa timu ya soka ya wanawake  ya Mkoa wa Mara Mara Queens  wakiwa  wanajifua jijini  Mwanza katika mazoezi makali kwa ajili ya kujiandaa na  mchezo wa marudiano  baina ya timu ya soka ya wanawake ya  Mkoa wa Mwanza  Mwanza Queens.


Star Tv imeshuhudia  wachezaji hao  wakifanya mazoezi hayo na kuelezea matumani yao katika mchezo wa marudiano Mkoani Mara huku wakilalamikia uongozi wa Mkoa wa Mara kwa kushindwa kuwasaidia vifaa vya michezo.
           
Katibu wa Mara Queens  Sure Mugeta  amesema  wameweka kambi  jijini  Mwanza kutokana na kudhaminiwana  na  mdau wa michezo ambaye ni m kurugenzi wa kituo cha michezo cha Alliance James Bwire na kutoa wito kwa wadau wengine wa Mkao  wa Mara kuiga mfano  huo kwa kutoa msaada wa hali na mali ili waweze kufanya vizuri zaidi.

Kocha Mkuu wa timu hiyo Msakato Magai amesema anauhakika wakufanya vizuri katika mchezo wa marudiano kutokana na mazoezi ambayio wameyafanya na wachezaji wake wote wako vizuri.
         
Katika mchezo wa  kwanza wa ufunguzi  wa kuwania kombe la Taifa la wanwake  baina ya Mara Queens  na Mwanza Queens  timu hiyo ilichpwa mabao sita kwa moja  na  mchezo wa  marudiano baina ya timu hizo unapigwa  katika uwanja wa Karume mjini Musoma  January 13 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment