WILSON KOLINA ELISHA

WILSON KOLINA ELISHA

BLOG HII NI MUHIMU KWA JAMII KUTOKANA NA KUJIKITA KATIKA KUANDIKA HABARI TOFAUTI ZA UHAKIKA NA ZILIZOFANYIWA UCHAMBUZI WA KINA...........

Monday, January 12, 2015

ZIARA YA RAIS WA TFF KATIKA KITUO CHA MICHEZO CHA ALLIANCE MWANZA

Mbele ni Rais wa Shirikisho la soka nchini TFF  Jamal Malinzi na mwenyekiti wa chama cha soka mkoani Mwanza MZFA Jackson Songora facebook akiwa na ujumbe kamili wakielekea kwenye viwanja vya michezo vya kituo cha michezo cha Alliance wakati wa ziara yake ya kukagua viwanja hivyo.


Shirikisho la soka nchini TFF limeridhishwa na maandalizi ya viwanja vitakavyotumika katika mashindano ya Taifa ya soka la vijana walio chini ya umri wa miaka 13.

Rais wa Shirikisho hilo Jamal Malinzi ametoa kauli hiyo jijini Mwanza  baada ya kukagua viwanja vya michezo vya Alliance ambavyo vitatumika katika mashindano hayo ambayo yamepangwa kufanyika jijini Mwanza Aprili Mosi  mwaka huu.

Kauli ya Rais wa Shirikisho la soka nchini TFF Jamal Malinzi  mara baada ya  ziara yake ya kukagua viwanja vya michezo katika kituo cha michezo cha Alliance cha jijini Mwanza.

Malinzi amesema kuwa  mashindano ya  soka ya Taifa ya vijana yana  umuhimu  wake hivyo  ni vema wadau wa soka kwa ujumla wakaunga mkono  jitihada zinazofanywa na kituo cha michezo cha Alliance.
           
Katika hatua nyingine Rais huyo ameonywa viongozi wa vyama vya soka vya mikoa kutoanda a vijana wenye umri mkubwa tofauti na wale waliochini ya umri wa mika 13 katika mashindano hayo.

Amesema kuwa lengo la mashindano hayo ni kuunda timu ya Taifa ya vijana ambao wataweka kambi ya mika mne kabla ya kuanza kwa  mashindano ya AFCON
 mwaka 2019 

          
Mkurugenzi wa kituo cha michezo cha Alliance  James Bwire amesema kufuatia ziara ya Rais wa  Shirikisho la soka nchini TFF Jamal Malinzi  katika kituo hicho wataendelea kufanya marekebisho  ya liyobaki  katika viwanja hivyo.

Kutokana na umuhimu huo mkurugenzi wa Alliance amemuomba Rais wa TFF kumuagiza mtaalam wa kutengeneza viwanja vya michezo kuja jijini Mwanza kwa ajili ya kusaidia marekebisho ya viwanja hivyo kabla ya kuanza kwa mashindano ya vijana waliochini ya umri wa miaka 13.
Malengo ya mashindano ya soka kwa vijana waliochini ya umri wa miaka 13 ni kuunda timu ya Taifa ya vijana ambayo itaweka kambi ya mika mine kabla ya kushiriki mashindano ya AFCON  mwaka 2019 ambapo Tanzania inatarajiwa kuwa mwenyeji wa mashindano hayo.
Sehemu ya wajumbe walioambatana na Rais wa TFF Jamal Malinzi wakiteta jambo furani wakati wakikagua viwanja vya michezo vya Alliance ambavyo vitatumika katika mashindano yaTaifa ya  soka ya viajana   Aprili Mosi mwaka huu.


 Miongoni mwa viwanja vya kituo cha michezo cha Alliance cha jijini Mwanza ukiwa upendwa nyasi.
Uwanja huu pia unaandaliwa kwa ajili ya kutumika kwa mashindano ya Taifa ya soka ya vijana ambayo yatashirikisha mikoa ya Tanzania

Rais wa TFF Jamal Malinzi akiwa na ujumbe wake wakati wa ziara ya kukagua maendelea ya maandalizi ya viwanja katika kituo cha michezo cha Alliance jijini Mwanza

Add caption



Kulia ni Mkurugenzi wa kituo cha michezo cha Alliance cha jijini Mwanza James Bwire akiowaelekeza wajumbe wa walioambatana na Rais wa TFF Jamal malinzi wakati wa ziara yake katika kituo hicho.


No comments:

Post a Comment