MKUU wa Mkoa wa Mwanza Magesa Mlongo amezindua mashindano ya soka ya Malando Cup katika kata ya Hung'humalwa wilayani Kwimba.
Akizungumza baada ya kuzindua mashindano hayo amesema anatambua kuwa lipo tatizo la ukosefu wa
viwanja vya michezo na vifaaa vya michezo katika maeneo mbalimbali Mkoani Mwanza jambo ambalo ni moja ya sababu zinazochangia kazi ya
kuvumbua, kukuza na kuendeleza vipaji vya wanamichezo kutofanyika kwa ufanisi.
Kutokana na hali hiyo
wadau wanapaswa kuona umuhimu wa kushiriki kikamilifu katika kukabiliana na
tatizo hilo ambalo linawafanya vijana wengi washindwe kuonyesha vipaji vyao huku Taifa likikosa wanamichezo wanaoweza kuiweka nchi katika ramani ya dunia katika michezo
Amesema michezo haijengi uadui, bali hujenga undugu, urafiki na huimalisha mahusiano, baina ya wanamichezo na viongozi, hivyo ni vema ikatumika kwa malengo ambayo yamekusudiwa
Aidha Mkuu huyo analiona suala la zawadi kuwa nila muhimu na
kuahidi kuwazawadia washindi wa tatu wa
juu katika timu zinazoshiriki mashindano hayo ambapo bingwa wa michuano
hiyo atajinyakulia kitita cha shilingi Laki mbili huku mshindi wa pili
akijipati shilingi Laki moja na nusu mshindi watatu ataambulia shilingi
Laki moja.
Amesema michezo haijengi uadui, bali hujenga undugu, urafiki na huimalisha
mahusiano, baina ya wanamichezo na
viongozi, hivyo ni vema ikatumika
kwa malengo ambayo yamekusudiwa
Mdhamini wa
mashindano
hayo Shija Malando anasema ameamua kuanzisha mashindano hayo ambayo
anaamini yatakuwa chachu kwa vijana na wakazi wa kata hiyo.
Ameongeza
kuwa baada ya kumalizika kwa mashindano hayo anatarajia kuanzisha
mashindano mengine aqmbayo atawashirikisha wazee katika mchezo wa bao,
wakimbiza baiskeli, mchezo wa wavu na wanawake kwa uapnde wa soka na
mchezo wa Netiboli.
"Hiyo
ni mikakati yangu ya badaye ambayo nina imani wilaya nzima ya Kwimba
itaiga mfano ambao nimeuanzisha kwa kufufua michezo ya aina tofauti,"
amesema Malando
Mashindano hayo yenye lengo la kuuaga mwaka 2014 na kuukaribisha mwaka
2015 yanazishirikisha timu nane za soka ambazo ziko kata ya Hung’humalwa wilaya ya Kwimba mkoani
Mwanza.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Magesa Mlongo akikagua timu za soka wakati wa ufunguzi wa Malando Cup 2014/ 2015 |
Mkuu wa wilaya ya Kwimba Seleman Mzee akionyesha baadhi ya vipaji vya wanamichezo katika mchezo wa ufunguzi wa kuwania Malando Cup 2014/2015 |
Sehemu ya jukwaa kuu wakiwa wanatazama kwa umakini jinsi mchezo wa ufunguzi unavyoendelea katika uwanja wa Mnadani kata ya Hung'humalwa. |
Kulia ni mdhamini wa mashindano hayo Shija Malando alipokuwa anatoausia kwa baadhi ya wanamichezo wa timu zinazoshiriki mashindano hayo |
Sehemu ya mashabiki wa sok awaliofurika katika uwanja wa Mnadani kushuhudia mchezo wa ufunguzi wa mashindano ya Malando Cup |
No comments:
Post a Comment