WILSON KOLINA ELISHA

WILSON KOLINA ELISHA

BLOG HII NI MUHIMU KWA JAMII KUTOKANA NA KUJIKITA KATIKA KUANDIKA HABARI TOFAUTI ZA UHAKIKA NA ZILIZOFANYIWA UCHAMBUZI WA KINA...........

Thursday, January 15, 2015

JAMII INAPASWA KULINDA MIUNDO MBINU INAYOJENGWA

Jamii inapaswa kulinda miundo mbinu inayojengwa katika maeneo yao ili kuweza kufikia malengo yaliyopangwa katika harakati za kukabiliana na changamoto zilizopo.








Baadhi ya miundo mbinu ya maji katika wilayani Nyang'hwale Mkoani Geita ikiwa imeharibika


Mwenye shati nyeusi  ni mkurugenzi wa Blog hii akifanya mahojiano na mkazi wa Kharumwa wilayani Nyang'hwale Mkoani Geita Bw. Henry Wilson juu ya hali  ya upatikanaji wa maji. 


Upo usemi usemao kuwa kazi ni kazi bora mkono uende kinywani ilimradi kazi hiyo iwe halali.  Huo ni usemi ambao watu  wengi wanashindwa kuutafisri vizuri na hivyo kuendelea kulalamikaii.

Hiyo ni kauli ya Henry Wilson mkazi wa Kharumwa akielezea jinsi anavyonufaika na shughuli ya kuchota maji .

Henry alisema kuwa kazi ya kuchota maji anaifanya kila siku na ameifanya zaidi ya miaka mitano ambapo ndoo moja ya lita ishirini anauza shilingi mia mbili hamsini wakati wa masika huku wakati wa kiangazi anauza ndoo moja kwa kiasi cha shilingi 1000.

Amebainisha kuwa kwa siku anauwezo wa kuuza zaidi ya ndoo 70 kwa wateja wake ambao

 Amesema kutokana na kazi hiyo ameweza kujjenga nyumba na anaitunza familia yake vizuri na ameahidi kuendelea kufanya kazi hiyo kwani ina manufaa zaidi.

Hata hivyo amelalimikia kitendo ambacho watu wasiojulikana waliweza kuharibu miundombinu ya maji na kutoa wito kwa ngazi husika kufanya kila jitihada kuwabaini wahusika ili wachukuliwe hatua za kisheria.

Kutokana na vijana wengi kukaa kijiweni bila kufanya kazi ametoa wito kuachana na tabia hiyo na badala yake wawajibike ili wajikwamue na umaskini na wasibague kazi.

Mwisho

No comments:

Post a Comment