WILSON KOLINA ELISHA

WILSON KOLINA ELISHA

BLOG HII NI MUHIMU KWA JAMII KUTOKANA NA KUJIKITA KATIKA KUANDIKA HABARI TOFAUTI ZA UHAKIKA NA ZILIZOFANYIWA UCHAMBUZI WA KINA...........

Thursday, February 13, 2014

ONGEZEKO LA WATU WENYE DHAMBI DUNIANI WACHUNGAJI WAASWA KUTUMIA MAANDIKO KWA USAHIHI.

WACHUNGAJI                                                                                             
Na Wilson Elisha
Mwanza

Wachungaji  wa  madhehebu ya  dini nchini  wameaswa kuyatumia maandiko matakatifu ya Mungu kwa usahihi kuwafundisha wanadamu  ili waweze kutenda mema na kuepusha maovu  yanayochangia  ongezeko la watu wenye dhambi duniani.

Akihubiri katika mahafali ya sita ya chuo kikuu cha Mount Meru cha kanisa la Baptist tawi Mwanza,   mchungaji Joseph Kahindi amesema kuwa wachungaji bado wanayo nafasi kubwa ya kubadili maisha ya wanadamu kuacha  maovu.

Amesema kuwa hatua hii itasaidai wanadamu kuepukana na dhambi ambazo mwisho wake ni mauti jambo ambalo ni hatari miongoni mwa jamii.

Mchungaji Kahindi ambaye pia ni mkuu  wa kitengo cha Theolojia katika chuo kikuu cha Mount Meru amesema  ni vema wachungaji wakazingatia maadili ya kiuchungaji katika kuwafundisha wanadamu ambao wamelemewa na mzigo wa dhambi.

Amesema hivi sasa ulimwengu umekubikwa na majanga mbalimbali ambayo yanachangia mmomonyoko wa maadili kwa wanadamu kuwa mkubwa na kujiingiza katika vitendo vya kumuasi Mungu.

Amefafanua kuwa kutokana na kuhitimu wachungaji ni muhimu wakitumia elimu waliyoipata katika kuwakomboa wanadamu ili wasiendelee kuangamia na dhambi.

Awali mwangalizi wa makanisa ya Baptist kanda ya ziwa mchungaji Boniphace Mponeja alielezea juu ya mchango unaotolewa na wachungaji katika jamii.

Alisema kuwa wachungaji wanapaswaa kuwa mstari wa mbele katika kufanya kazi kwa umakini kwani kazi inamjengea heshima mwanadamu sanjari na kujitafutia riziki halali.

Mkurugenzi mkazi nchini kutoka Chuo kikuu cha Mount Meru Nancy Giddens amesema jukumu walilonalo ni kutoa elimu kwa wachungaji ili waweze kujikita katika kuwafundisha wanadamu.

 Mkurugenzi mkazi huyo alisema kuwa licha ya changamotoi zilizopo katika kuwafundisha wachungaji na wake wa wachungaji lakini bado uongozi wa Chuo kikuu cha Mount Meru unaendelea kujitahidi ili kuepukana na chnagmoto hizo.

Katika mahafali hayo ya sita ambayo yamefanyika katika kanisa la Baptist jijini Mwanza wachungaji 21 wametunukiwa vyeti bada ya kuhitimu na kufuzu masomo ya THEOLOJIA,  huku wake wa chungaji 16 wakitunukiwa vyeti vya biblia na huduma ya kikristo.




No comments:

Post a Comment