WILSON KOLINA ELISHA

WILSON KOLINA ELISHA

BLOG HII NI MUHIMU KWA JAMII KUTOKANA NA KUJIKITA KATIKA KUANDIKA HABARI TOFAUTI ZA UHAKIKA NA ZILIZOFANYIWA UCHAMBUZI WA KINA...........

Saturday, January 11, 2014

ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 18 KUTUMIKA KATIKA MRADI WA WAZAZI NA MWANA



WILSON ELISHA
MWANZA


Zaidi ya shilingi Bilioni 18  zinatarajia kutumiwa na Serikali za Tanzania na Canada katika kutekeleza mradi wa  miaka mitatu na nusu wa Wazazi na Mwana unaotekelezwa katika wilaya  tano za mikoa ya Mwanza na Rukwa.

Meneja wa mradi huo Dokta Safila Telatela alisema hayo baada ya kukabidhi simu za mkononi  kwa mkuu wa wilaya ya Ilemela mkoani Mwanza Amina Masenza katika hafla fupi iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa manispaa ya Ilemela 

Alibainisha kuwa mradi huo unatarajiwa kuwanufaisha zaidi ya watu milioni moja wakiwemo wanawake zaidi ya laki tatu wenye umri wa kujifungua watoto, wanaume themenini elfu,  watoto zaidi ya laki tatu na kuwajengea uwezo wafanyakazi zaidi ya elfu moja, sanjari na wanajamii wapatao laki tano wa kujitolea katika vijiji 516.

 Aidha meneja huyo alisema kuwa mradi unalenga kupunguza vifo vya akinamama wajawazito, watoto wachanga na walio chini ya miaka mitano ambavyo vimekuwa vikitokea katika maeneo mbalimbali nchini yakiwemo ya mradi. 

Alifafanua kuwa mradi huo unatekelezwa katika wilaya za Ilemela na Sengerema mkoani Mwanza, na wilaya za Nkasi, Sumbawanga vijijini na Kalambo mkoani Rukwa utahakikisha unasaidia kuwasomesha madaktari na wauguzi watakaofanya kazi katika vituo vya afya vitakavyotoa huduma ya upasuaji.

Alisema kuwa hivi sasa ujenzi wa vyumba vya upasuaji katika vituo vya afya vya mwangika na Sangabuye unaendelea na kwamba utakapo kamilika vitatolewa vifaa vya kiusasa kwa ajili ya kuwahudumia wagonjwa watakaopatiwa huduma ya uapasuaji. 

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Ilemela Amina Masenza mkoawa Mwanza Amina Masenza alisema kutolewa kwa simu hizo kutaboresha rufaa za wagonjwa na kusaidia katika mawasiliano ya haraka pale ambapo ushauri wa haraka unatakiwa ili kuokoa maisha ya wagonjwa.

"Ninaamini simu zilizotolewa zitafanya kazi iliyokusudiwa ili malengo  yaweze kutimia hususani kuoka maisha ya mama wajawazito, watoto wachanga na watoto chini ya miaka mitano,"alisema mkuu wa wilaya

"Sitegemei, sitarajii mtumishi yeyote aondoke na simu halafu aliyepozamu ahangaike kupata mawasiliano ya haraka kwa ajili ya wagonjwa watakaokuwepo katika vituo vya kutolea huduma," aliongeza mkuu huyo

Alibainisha kuwa mradi unafanya kazi katika vituo vya kutolea huduma vipatavyo 74 katika wilaya za Sengerema na Ilemela ambapo wilaya ya Ilemela inavituo 15 wakati wilaya ya Sengerema ina vituo 59.

Katika mradi huo tayari vituo vya afya vya Mwangika wilayani Sengerema na Sangabuye wilayani Ilemela vimekwisha patiwa magari ya kubebea wagonjwa. 

Mradi huu unafadhiliwa na serikali ya CANADA kwa kushirikiana na serikali ya Tanzania na unatekelezwa na mashirika matatu yasiyo ya kiserikali ambayo ni Plan International, Africare na Jhpiego na unatarajia kufikia tamati Aprili mwaka 2015.

Mwisho


     


No comments:

Post a Comment