WILSON KOLINA ELISHA

WILSON KOLINA ELISHA

BLOG HII NI MUHIMU KWA JAMII KUTOKANA NA KUJIKITA KATIKA KUANDIKA HABARI TOFAUTI ZA UHAKIKA NA ZILIZOFANYIWA UCHAMBUZI WA KINA...........

Wednesday, April 22, 2015

MFUKO WA MAENDELEO YA JAMII TASAF WATOA MAFUNZO


Kaimu Mkurugenzi msaidizi wa TASAF Chrisopher Sanga akitoa hotuba ya ufunguzi katika  kikao kazi cha waratibu wahasanibu na Maafisa wa ufuatiliaji wa mpango wa kunusuru kaya maskini na waandishi wa habari kutoka mikoa ya Geita , Kagera na Shinyanga ambacho kimefanyika jijini Mwanza  
USHIRIKISHWAJI wa jamii na wadau mbalimbali katika mpango wa kunusuru kaya maskini nchini ni moja kati ya misingi ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF katika kuhakikisha walengwa wananufaika na mpango huo.

Kauli hiyo imetolewa na Kaaimu Mkurugenzi Mkuu msaidizi  wa TASAF Chrisopher Sanga kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa mfuko huo Laudslaus Mwamanga wakati wa ufunguzi wakikao kazi kwa waratibu wahasibu  wa mpango  maafisa ufuatiliaji nawaandishi w ahabari kutoka mikoa ya Kagera, Shinyanga na Geita.

Baadhi ya waandishi wa habari ambao wameshiriki kikao kazi katika harakati za kunusru kaya maskini
Amesema kuwa kuwepo kwa kikao hicho anauhakika kwa kiasi kikubwa utasaidia zaidi kuimarisha mahusiano ya kiutendaji baina ya Mfuko huo walengwa na Taasisi za habari katika maeneo ya utekelezaji wa shughuli za mpango wa kunusuru kaya maskini katika mikoa husika.
 
Baadhi ya waratibu wahasibu na maofisa ufuatiliaji wa mpango wa TASAF wakisikiliza mada katika kikao kazi pamoja na waandishi wa habari

Ameongeza kuwa mafanikio ambayo yamekwisha patikana katika awamu hii ya tatu yametokana na ukweli kwamba ni ushirikiano uliopo baina ya watendaji na wanahabari katika utoaji wa habari zinazohusu nfuko huo kwa 

Pamoja na mafanikio hayo bado kuna changamoto zilizopo kuhakikisha kaya masikini  zinajikwamua hivyo kunahitajika maboresho zaidi.


Amebainisha kuwa TASAF ni chombo cha serikali kama mojawapo ya jitihada za kupunguza umaskini kwa kushirikiana na vyombo vingine vilivyopo.
Zuhura Mdungi Mkuu wa Kitengo cha Habari TASAF akitoa ufafanuzi wa jambo furani kwa washiriki wa kikao kazi

Katika kikao hicho mada mbalimbali zimeweza kuwasilishwa ikiwemo uhaulisaji  fedha  na kimewashirikisha waratibu , wahasibu  wa mpango maafisa ufuatiliaji na waandishi wa habari kutoka mikoa ya Shinyanga, Geita na Kagera.

No comments:

Post a Comment