WILSON KOLINA ELISHA

WILSON KOLINA ELISHA

BLOG HII NI MUHIMU KWA JAMII KUTOKANA NA KUJIKITA KATIKA KUANDIKA HABARI TOFAUTI ZA UHAKIKA NA ZILIZOFANYIWA UCHAMBUZI WA KINA...........

Saturday, October 31, 2015

BODI YA MAJI JIJINI MWANZA MWAUWASA YAFANYA ZIARA YA KUTEMBELEA MIRADI



MWAUWASA BODI
Na Wilson Elisha
Mwanza


 Zaidi ya kiasi cha shilingi Milioni   mia saba zinaendelea kutumika  kwa ajili ya  kunusuru kero ya upatikanaji wa maji safi na salama  kwa wananchi waishio katika maeneo ya mlimani jijini Mwazna

Hii itasaidia miundo mbinu inayojngwa  kuwa endelevu kwa kizazi  cha sasa na kijacho  katika kutatua changamoto zinazowakbili wananchi wa maeneo mbalimbali  

Ni moja ya ziara ya wajumbe wa bodi ya wakurugenzi  wa Mamlaka ya Maji safi na usafi wa Mazingira jijini Mwanza MWAUWASA ya kukagua miradi ya maji  inayotekelezwa

Mkurugenzi  mtendaji  wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa mazingira  MWAUWASA  Mhandisi Anthon Sanga  amesema kuwa licha ya changamoto za upatikanaji wa maji safi na salama  jijini Mwanza lakini zipo jitihada zinazofanywa


 Mhandisi Sanga amesema kuwa kutokana na kuanza kujengwa kwa miradi ya dharura ya kunusuru hali ya upatikanaji wa maji  anamini katika kipindi cha mwezi mmoja kuanzia sasa wananchi waishio katika maeneo ya mlimani wataanza kunufaika na mradi huo


Mwakilishi wa Wizara ya Maji ambaye ni Mjumbe wa bodi ya maji jijini Mwanza MWAUWASA Mhandisi Paschal Hamuli amesema kuwa serikali itaendelea na jitihada za kuhakikisha wananchi wanapata maji safi na salama ili kuondoa kero inayowakabili


Baadhi ya wajumbe wa bodi ya maji  MWAUWASA ambao  wamejionea hali halisi ya  namna ambavyo ujenzi wa miundombinu ya maji unavyoendelea hawakusita kuelezea furaha yao licha ya changamoto zilizopo


Katika kutatua kero ya maji kwa wananchi  Mamlaka ya Maji safi na usafi wa mazingira jijini Mwanza MWAUWASA  wameanzisha miradi ya dharura kwa kuweka pampu ya kusukuma maji kwenda katika  baadhi ya  maeneo

Mwisho
************************************************

No comments:

Post a Comment