WILSON KOLINA ELISHA

WILSON KOLINA ELISHA

BLOG HII NI MUHIMU KWA JAMII KUTOKANA NA KUJIKITA KATIKA KUANDIKA HABARI TOFAUTI ZA UHAKIKA NA ZILIZOFANYIWA UCHAMBUZI WA KINA...........

Tuesday, October 13, 2015

IDADI YA WAZEE DUNIANI YAZIDI KUONGEZEKA




Inakadiriwa kuwa ifikapo mwaka 2050 idadi ya wazee kuanzia miaka 60 na kuendelea duniani na Tanzania  ikiwemo  itafikia  zaidi ya  Bilioni mbili ambayo ni sawa na asilimia 21.5 ya watu wote duniani

Hayo yamebainishwa na Naibu Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la HelpAge International  Tanzania, Smart Daniel wakati akifungua mkutano wa wadau wanaojihusisha na kulinda na kutetea haki za wazee nchini,  wahariri wa vyombo vya habari na  waandishi wa habari unaoendelea jijini Dar es Salaam 

Mkurugenzi huyo amesema kuwa kutokana na hali hiyo  ipo haja ya kufanya  jitihada za maksudi za  kuhakikisha sera ya wazee ya mwaka 2003 inatungiwa sheria ili wazee hapa nchini waweze kutambuliwa kisheria vinginevyo wazee wataendelea kukabiliwa na  changamoto  nyingi ikiwemo ya ukosefu wa  huduma bora za Afya 

Ameongeza kuwa hii ni kutokana na  ukweli kwamba  hivi sasa kuna zaidi ya wazee Milioni Mbili na Nusu nchini   idadi ambayo inazidi kuongezeka kila kukicha  wakati hakuna mipango yoyote yenye tija kwa wazee hao 


Naibu Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la HelpAge International  nchini Smart Daniel akifungua mkutano huo amesema kuwa  wazee wanakabiliwa na changamoto nyingi licha ya kuwa idadi ya wazee inazidi kuoingezeka  jambo linalohitaji nguvu ya pamoja


Aidha Daniel ameelezea idadi ya watu duniani waliopo  hivi sasa na katika kipindi cha miaka  35 ijayo  huku akitolea mfano nchi ya Japan ambayo imeweza kujipanga vizuri katika kuwashughulikia wazee ambapo zaidi ya asilimia 30 wanahudumiwa kikamilifu ikilinganishwa na hapa nchini asilimia nne wapo katika mifuko ya hifadhi ya jamii



Akizungumzia  suala la afya kwa wazee  Afisa  Miradi ya Afya  na Uwezeshaji wa  kipato kwa wazee wa shirika la HelpAge International  Leonard Ndamugoba  amesema kuwa  bado huduma ya afya kwa wazee  ni tatizo huku mratibu wa kitengo cha Haki na Sheria  kutoka HelpAge Joseph  Mbasha amesema takwimu za mauaji ya wazee zinazidi kuongeka





Baadhi ya wadau na waandishi wa habari katika mkutano huo wamesema kuwa changamoto zinazowakabili wazee zipo katika maeneo mbalimbali ikiwemo miundombinu ya barabara  ambayo ni kwazo kwa wazee katika kupata huduma za afya

Kwa upande wake mdau kutoka Shirika la MAPERECE la wilayani Magu mkoani Mwanza Julius Mwengela amesema kuwa licha ya changamoto hizo zipo jitihada zinazofanywa na shirika lake pamoja na jeshi la Polisi mkoani humo kwa kutoa elimu kwa waganga wa jadi

Naye mwandishi wa habari wa Star Tv na Radio Free Afrika mkoani Ruvuma Adam Nindi amesema kuwa waandishi wa habari wanaowajibu wa kuandika habari zinazohusu wazee kwani wao ni sehemu ya jamii


Mkutano huo  umewashirikisha  wadau wanaojihusisha na kulinda na kutetea haki za wazee ,  waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini na  maafisa ustawi wa Jamii wa wilaya na vijiji na  umeandaliwa na Shirika la Help Age International

Mwisho

*********************************




No comments:

Post a Comment