WILSON KOLINA ELISHA

WILSON KOLINA ELISHA

BLOG HII NI MUHIMU KWA JAMII KUTOKANA NA KUJIKITA KATIKA KUANDIKA HABARI TOFAUTI ZA UHAKIKA NA ZILIZOFANYIWA UCHAMBUZI WA KINA...........

Friday, November 27, 2015

ZIARA YA NAIBU KATIBU MKUU WIZARA YA MAJI MWAUWASA JIJINI MWANZA

Wa pili kutoka kulia ni Naibu katibu mkuu Wizara ya Maji Mhandisi Ngosi Mwihava  akijadiliana jambo na mbunge wa Jimbo la Ilemela Mheshimiwa Angelina Mabula mwenye kitenge na watumishi wa MWAUWASA akiwemo mkurugenzi mtendaji wa MWAUWASA akiwemo mkurugenzi mtendaji mhandisi  Anthony Sanga  mwenye suti nyeusi aliyegeuka kuangalia jengo




 Mwenye suti nyeusi  ni mkurugenzi mtendaji wa MWAUWASA Mhandisi Anthony Sanga akiwa na baadhi ya wajumbe wa bodi ya Mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira jijini Mwanza MWAUWASA wakati wa ziara ya Naibu katibu mkuu wizara ya Maji

 Watatu kutoka kulia mwenye suti ni Naibu katibu Mkuu Wizira ya Maji Mhandisi Ngosi Mwihava akijadiliana jambo furani na mhandisi Anthony Sanga mkurugenzi mtendaji wa MWAUWASA  wa pili kutoka kushoto huku wapili kutoka kulia ni Mbunge wa Jimbo la Ilemela Mheshimiwa Angelina Mabula


 Mbunge wa Jimbo la Ilemela Mheshimiwa Angelina Mabula akijadiliana na mmoja wa wahandisi wa MWAUWASA


Naibu katibu mkuu Wizara ya Maji  Mhandisi Ngosi mwihavawa kwanza kutoka  kulia akikagua moja ya majengo ambayo yamejengwa kwa ajili ya kuhifadhia mashine za kusukuma maji kuelekea katika maeneo ya milima na miinuko

Licha ya  maeneo mengi nchini Tanzania kuzungukwa na vyanzo vya maji,bado maeneo hayo yanatajwa kukabiliwa na uhaba wa maji hasa wanaoishi  maeneo ya milima na  miinuko,



Hata hivyo jukumu la serikali linatajwa kuhakikisha maeneo hayo yanapatiwa huduma ya maji safi na salama kwa kuzingatia malengo ya meliniamu ya kuhakikisha maeneo ya mjini yanapatiwa huduma hiyo kwa asilimia 95 na vijijini asilimia 85 ifikapo mwaka 2020.



Jiji la Mwanza ni moja ya maeneo yanayokabiliwa na matatizo ya upatikanaji wa maji safi na salama hasa katika meneeo yenye milima na miinuko



Kutokana na changamoto hiyo inayowakabili wananchi  Naibu katibu mkuu wa Wizara ya Maji Mhandisi  Ngosi Mwihava amefanya ziara ya kutembelea baadhi ya miradi inayotekelezwa na Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira jijini Mwanza MWAUWASA


Eneo la Isamilo na mji mwema ni kati ya maeneo yaliyopo milimani ambayo   yamekuwa yakikabiliwa na uhaba wa maji kwa muda mrefu  sasa ni mwanzo wa maisha mapya ya furaha kupata maji yaliyo safi na salama.


Mhandisi Anthony Sanga ambaye ni mkurugenzi mtendaji  wa MWAUWASA na Mhandisi Abbas  Muslim Meneja mradi  MWAUWASA wamesema kuwa miradi yote inayotekelezwa na MWAUWASA ina lenga kutataua uhaba wa ,maji kwa kipindi kifupi ingawa upo  mradi mkubwa ambao unatarajiwa  kutataua kero hiyo katika maeneo mengi



Hata hivyo Wabunge wa majimbo ya Nyamagana na Ilemela mkoani Mwanza Angelina Mabula na Stanslaus Mabula wameiomba  serikali  kuisaidia Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira jijini Mwanza MWAUWASA ili iweze kuondoa kero ya upatikanai wa maji safi na salama  inayowakabili wananchi



Naibu katibu Mkuu wa Wizara ya Maji Mhandisi Ngosi Mwihava amefafanua  hoja za wabunge hao kuwa serikali inatambua  mbali ya   kuwa maji ni uhai pia ni sehemu ya  uchumi  hivyo suala hilo litafanyiwa kazi kadri itakavyowezekana





Ziara hiyo ya Naibu katibu mkuu wa Wizara ya Maji  imehitimishwa kwa kutiliana saini ya mkataba wa  makubaliano ya mkopo wa fedha za utekelezaji wa miradi ya maji inayofadhiliwa na Benki ya maendeleo ya Ujeruman KFW



Mwisho

**************************


No comments:

Post a Comment