WILSON KOLINA ELISHA

WILSON KOLINA ELISHA

BLOG HII NI MUHIMU KWA JAMII KUTOKANA NA KUJIKITA KATIKA KUANDIKA HABARI TOFAUTI ZA UHAKIKA NA ZILIZOFANYIWA UCHAMBUZI WA KINA...........

Saturday, December 26, 2015

TAASISI YA BILAL MUSLIM MISSION YATOA MATIBABU BURE KWA WAGONJWA WA MACHO MWANZA


Mratibu wa kambi ya macho kutoka Taasisi ya Bilal Muslim nchini Tanzania Ain Ashaff alielezea juu ya matibabu hayo kwa wagonjwa wa macho  

Wakati  idadi ya wagonjwa wa macho nchini ikizidi kuongezeka kila kukicha zimetajwa sababu mbali mbali ikiwemo chakula  huku zaidi ya wagonjwa 300 wenye matatizo hayo mkoani Mwanza wanatarajiwa kufanyiwa upasuaji wa macho kati ya  wagonjwa 5000 watakaopatiwa  matibabu hayo na Taasisi ya Bilali Musilim Mission ya nchini Tanzania.

 Matibabu hayo yanayotolewa na  jopo la madaktari bingwa wa  huduma za  upasuaji wa  magonjwa  ya macho ni ishara tosha kuwa ni mkombozi wa utatuzi wa magonjwa hayo  ambayo imekuwa ni changamoto kubwa miongoni mwa jamii kutokana na kuwa na gharama kubwa.


Mwandishi Wilson Elisha ameandaa taarifa ifuatayo

NARRATION

Mzee Philimon Bashigwa mkazi wa Mkuyuni jijini Mwanza mwenye umri wa miaka 78 akiwa ni mmoja wananchi ambao wamefika kupata matibabu ya macho lakini yeye anasema huduma hiyo imefika mda mwafaka.

SB: Mzee Philimon Bashigwa – Makazi wa Mkuyuni

Baadhi ya wananchi waliofika katika klinki hii ya macho kwa ajili ya kupata matibabu huku kundi kubwa wakiwa ni wazee na wanawake wanaonekana kujitokeza kwa wingi.

Madaktari bingwa waliobobea katika  suala la upasuaji macho wakiwajibika katika majukumu yao ili kufaniksha matibabu kwa wagonjwa wa macho.

Mratibu wa kambi ya macho kutoka Taasissi ya Bilal Muslim Misheni ya nchini Tanzania Ain sharif akiongea wakati wa zoezi la upimaji amesema kuwa lengo ni kuona watanzani wanaondokana na tatizo hilo.

SB: Ain Shariff Mratibu Kambi ya Macho Bilal Muslim Tanzania

Aidha Shariff amesema kuwa uapasuaji matibabu pamoja na dawa wanatoa bure japo kuwa wagonjwa wa upasuaji wanapelekwa katika Hospitali ya Sekoutoure hivyo  wakazi wa jiji la Mwanza amewataka kutumia fursa ya uwepo wa madaktari bingwa kijitokeza kwa wingi

SB: Ain Shariff  - Mratibu Kambi ya Macho Bilal Muslim Tanzania


Baadhi ya watu waliojitokeza kupata huduma hiyo ya macho wameiomba Taasisi hiyo kujenga utamaduni wa kutoa huduma hiyo  ili kusaidia watu wengi zaidi ambao wanasumbuliwa na ugonjwa wa macho

VOX 3
1.Mosses Messo -  Mgonjwa wa macho
2.Verediana Kileo – mgonjwa wa macho
3.Aman Abdallah  - Mgongwa wa macho

Taasisi ya Bilali Musilim misheni Nchini imekuwa ikishirikiana na taasisi za serikali katika kuihudumia jamii ili kukabiliana changamoto mbali mbali za kujiletea maendeleo

Taasisi hiyo imeshafikia baadh ya mikoa hapa nchi katika kutoa huduma ya macho kwa wagonjwa na hivyo huwawezesha wenye matatizo ya kutoona kuweza kuona.

Mwisho
***************

No comments:

Post a Comment